Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 31 Machi 2016

marafiki wa elimu musoma kutoa msaada kwa wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu

kutokana na dhana ya marafiki wa elimu ya kuhakikisha elimu bora kwa wanafunzi wote wa kitanzania, hivi karibuni mtandao wa marafiki wa elimu wameamua kujichangisha ili kuweza kukusanya vifaa vya shule kwa ajili ya kuweza kusaidia wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu.

mpango huo wa marafiki wa elimu umelenga kusaidia wanafunzi 25 vifaa vya shule kama madaftari,kalamu mabegi na sare za shule.
mpango huo utatekelezwa tarehe 15/04/2016
kwa mdau atakaeguswa na mpango huu anaweza kuwasiliana na marafiki wa elimu musoma kwa nambari 0755 650 075
katibu msaidizi wa marafiki wa elimu Kaseja january akisoma machapisho

rafiki wa elimu Juma okumu pamoja na Godfrey Mjaya wakisoma machapisho kabla ya kikao kuanza

mwenyekiti mpya wa mtandao wa marafiki wa elimu musoma Bi Perus masokomya

rafiki elimu Daniel Richard akipokea michango ya marafiki

Kaseja January akihakiki vifaa vilivyopatikana

katibu wa marafiki wa elimu musoma Bi Rose Olimo

mlezi wa mtandao wa marafiki wa elimu musoma thomas bega aliyesimama

marafiki wakimsikiliza mwenyekiti wa mtandao

mwenyekiti wa mtandao akizungumza na marafiki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni