Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Ijumaa, 20 Januari 2017

Pakua mpango mkakati wa haki elimu 2017/2021

Nadharia ya mabadiliko katika mpango Mkakati wa HakiElimu wa miaka mitano (2017- 2021). Nadharia hii inaonesha Dira tuliyonayo, matarajio tunayotegemea na jinsi ya kufika huko. Jipatie nakala ya mpango huu kwa lugha ya Kiswahili kwa kupakua kutoka katika link ifuatayo http://bit.ly/2iIzT2P

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni