Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 29 Mei 2018

Mkutano wa marafiki wa elimu Musoma






 Marafiki wa elimu musoma mapema siku ya jumamosi walikutana na kujadili changamoto zinazokabili elimu katika manispaa ya Musoma Mjini,

katika mkutano huo wa marafiki wa elimu, waliweza kubaini uwepo wa mimba nyingi kwa wanafunzi hasa wa sekondari ambazo haziripotiwi kwenye vyombo vya dora.
aidha marafiki hao wa elimu kwa pamoja waliaziamia kuanzisha mpango mahususi wa kutoa elimu kwa wanajamii, kwani imegundulika wazazi wengi wamekuwa chanzo cha mimba hizo kwa kuficha ukweli pindi watoto wao wapatapo ujauzito wakiwa shule.

.
picha matukio na, CIV Juma Okumu






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni