Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 9 Oktoba 2013

wanafunzi kidato cha pili wafanya mtihani

Dar es Salaam. Jumla ya watahiniwa 531,457 wa kidato cha pili wanatarajia kufanya mtihani utakaoanza kesho Oktoba 7 hadi 21 mwaka huu.Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome  alisema mitihani hiyo itafanyika kwa wiki mbili.
Alisema kati ya idadi hiyo, wasichana ni 270,734  sawa na asilimia 50.9 na wavulana ni 260,723 sawa na asilimia 49.1.Mchome alisema katika taarifa yake kwamba idadi ya shule na vituo vilivyosajiliwa kufanyia mtihani huo mwaka huu ni 4,437  ikiwa ni ongezeko la vituo 140 sawa na asilimia 3.3 ikilinganishwa na vituo 4,297 vilivyosajiliwa mwaka 2012.
Alisema watahiniwa waliojiandikisha wanajumuisha makundi maalum yenye uoni hafifu, ambao ni 89 na wasioona 93.ìKaratasi za mtihani wa watahiniwa wenye mahitaji maalum zimeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji yao kama vile kutumia karatasi za maandishi yenye nundu kwa wasioona na kuongeza ukubwa wa maandishi kwa wenye uoni hafifu,î alisema.
Mchome alisema umuhimu wa mtihani huo ni kupima kiwango cha maarifa na ujuzi alioupata mwanafunzi kutokana na mada alizojifunza katika kidato cha kwanza na cha pili.
Pia alisema mtihani huo unatoa changamoto zinazosaidia wanafunzi, walimu, wizara na wadau wa elimu kutambua mapungufu yaliyopo katika ufundishaji ili yaweze kufanyiwa marekebisho kwa lengo la kuboresha elimu.
chanzo. mwananchi.co.tz

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni