Tuhuma hizo ziliibuliwa na baadhi ya wazazi wa wanafunzi hao, wakisema wamechoshwa na ahadi za mwalimu huyo kwa zaidi ya miaka miwili sasa tangu vyeti hivyo kupotea, ziliandikwa na gazeti hili hivi karibuni.
Wazazi hao walidai mkuu huyo alihusika kwa sababu hakuwa wazi kueleza mazingira halisi ya jinsi vyeti hivyo vilivyopotea na kwamba hakupenda suala hilo lifike ngazi za juu.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, mwalimu huyo, alisema tofauti zilizojitokeza awali hadi kusababisha vyeti hivyo kuchelewa kukabidhiwa kwa wahitimu zimepatiwa ufumbuzi na vyeti hivyo vipo tayari.
Alisema baada ya mchakato wa kuviandaa vyeti hivyo kukamilika tangu juzi, klichobaki ni kuwakabidhi wahitimu hao.
“Mbona nimeanza kuwakabidhi wachache waliopata taarifa… nimeweka matangazo katika eneo linalozunguka shule kwa ajili ya kuwajulisha kuwa vyeti vyao vipo tayari ni wao wenyewe sasa.
“Niwaombe wazazi kupitia gazeti lenu wa waambie watoto wao waende shuleni hapo wakachukue vyeti vyao,” alisema Jasembe.
Hivi karibuni wazazi wa watoto hao, walifikisha tuhuma hizo kwa Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile, Ofisa Elimu na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni