Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 6 Februari 2014

Wizara sita kufanyiwa tathmini `Matokeo Makubwa Sasa`

Mfumo  wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) unatarajia kufanya tathmini katika wizara sita ili kuona ni kwa kiasi gani umefanya kazi na ripoti itakabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete na kuwekwa kwenye mitandao.

Mtendaji Mkuu wa mfumo huo chini ya Ofisi ya Rais, Omari Issa, alisema tathmini ya mwaka mmoja itafanyika na taarifa kuwekwa wazi ili kila wizara ijipime na kuona kama imefikia malengo husika.

Alisema pia Februari 24, mwaka huu kutakuwa na mkutano na wafanyabiashara lengo likiwa ni kuwapa uwanja wa kueleza vikwazo vya kufanya biashara vilivyopo nchini kwa sasa ambavyo vinalalamikiwa.

Alisema chini ya mfumo huo ambao unmelenga kutatua matatizo yanayokwamisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo wengi wamesingizia kukosekana kwa fedha jambo ambalo alisema siyo kweli.

“Katika tathmini hiyo watabainisha matatizo ya wizara hadi wizara, mradi hadi mradi, uchambuzi wa kina utaonyesha nani apewe kiasi gani kwa ajili ya kutekeleza lipi…awali wizara ilikuwa inapewa kulingana na bajeti hata kama hawazitumii kwa wakati huo, lakini kwa sasa watapewa kulingana na utekelezaji,” alisema Issa.

Alisema mfumo huo umeweka utaratibu thabiti wa kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa miradi katika maeneo ya kilimo, elimu, maji, nishati, uchukuzi na ufuatiliaji wa rasilimali, lengo likiwa ni kuwa na uwajibikaji wa kila mshiriki au taasisi katika utekelezaji wa miradi ya serikali ili kupata mafanikio haraka.

Kadhalika, Issa alisema mfumo umeanzisha kitengo cha kusimamia utekelezaji na ipo katika mchakato wa kuanzisha vitengo vya kusimamia utekelezaji katika ngazi za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa ili kuongeza ufanisi wa kutekeleza miradi katika ngazi zote.

“Ili kufanikisha BRN, tunahitaji ushirikiano wa sekta binafsi ambayo italeta teknolojia, utaalamu wa menejimenti na mtaji, ili kuhamasisha ushirikiano huo tumeanzisha mchakato wa kurazinisha mfumo na taratibu za ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) ili tuhakikishe inatoa mchango wake stahili katika utekelezaji wa BRN,” alisema.

Alisema maeneo ya kimkakati ya kitaifa ni usambazaji wa maji salama vijijini ambako kwa kipindi cha miezi sita zaidi ya watu 300,000 wamepata maji, ulinzi wa chakula, elimu ya msingi na sekondari, kuimarisha usafirishaji wa bandari, reli na barabara katika kanda ya kati, upatikanaji na uzalishaji na utafutaji wa rasilimali fedha.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni