Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 6 Februari 2014

serikali inachangia kuua elimu nchini

SERIKALI imekuwa kama haioni maovu yanayofanywa kienyeji na watendaji wake  ndani ya sekta ya elimu.
Na kama inaona basi inaamua kufumbia macho.
Novemba 7, 2012, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu, Majaliwa Kassim, alisema bungeni kuwa ni kosa walimu wakuu kutoza fedha kwa watoto wanaoanza darasa la kwanza, lakini tozo limekithiri.
Majaliwa alionya mwalimu atakayefanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria, agizo ambalo serikali yenyewe kupitia watendaji  linaonekana kupigwa mweleka, huku wazazi wakishangaa kuwapo michango isiyoeleweka na mingine ilikubalika kupitia kamati za shule.
Imefika mahali sasa inaonekana wazazi wanafahamu sana umuhimu wa watoto wao kusoma ili baadaye walikwamue taifa  na familia zao, lakini watendaji wa elimu husika wamekuwa mzigo na kikwazo cha watoto hao kupata elimu.
Hivi karibuni mkoani Morogoro, wazazi walifikia kupigana wakigombea watoto waandikishwe ili wasome, lakini mbali ya ugomvi huo, lalamiko na kikwazo kilichotajwa, ni tatizo la tozo na michango kwa wanaoandikisha kufikia sh 50,000 kwa mtoto.
Mbunge wa Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood, katika uandikishaji huo, aliingia katika suluba kutoa ufafanuzi ili kuondoa utata baina ya wazazi na waandikishaji, ambapo malipo  ya sh 50,000 kwa mtoto anayeandikishwa, kunaashiria wakuu wa shule kuwa na mradi wa kutumbua fedha kupitia uandikishaji.
Kwa kuwa Kassim alishatolea ufafanuzi, Mwalimu Mkuu au yeyote anayekiuka agizo la michango kuwa atachukuliwa hatua kali, basi kwa hali ilipofikia hadi wazazi wanapigana na wengi wao kukosa kuandikisha watoto wakitumia tozo feki, waadhibiwe.
Ninasema hivyo kwa sababu walimu wakuu wakisaidiana na watendaji wa vijiji na kata, wanaamua kufanya lolote kuhusu elimu bila kupata hata ushauri.
Siku hizi imekuwa si ajabu, walimu wakuu na waratibu wa elimu wakikosa mapato, basi wakilala na kuamka utakuta wanapanga mipango ya kuhakikisha wanapata fedha, mojawapo ikiwa ni kutumia uandikishaji wa wanafunzi kama mradi wa kujipatia fedha.
Bila kufahamu uwezo na kipato cha wananchi wa hali ya chini, wamekuwa wakiwakandamiza na kuwanyanyasa wananchi, na wakati mwingine wanafikia kuwaweka ndani eti kwa sababu ya kushindwa kulipa michango hiyo.
Hapa ndipo ninaposema, aibu ya elimu Tanzania tujifiche wapi? Maana udhaifu wa sekta hii na mipango yake mibovu, haionyeshi mpango mkakati wowote unaowekwa ili kuwe na uwazi wa kuandikisha wanafunzi.
Ni mara nyingi tumeona walimu wakuu na waratibu wa elimu, wamekuwa tatizo kwenye elimu ndani ya vitongoji, vijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa na taifa, ambapo watendaji wamekuwa wakiamua mambo wanavyotaka bila kuwa na vigezo huku wazazi wakiteseka.
Tatizo jingine linalosababisha malumbano sekta ya elimu, ni Kamati za shule ambazo zimekuwa mizigo zikishirikiana na wakuu wa shule, kiasi kwamba wanakaa kupanga mambo wakiangalia uwezo na mishahara waliyonayo bila kutazama kipato cha wananchi.
Ifike mahali hawa nao wasifumbiwe macho maana badala ya kuwa kioo ndani ya elimu, wamekuwa giza kwenye elimu hiyo.
Hawana mbinu na mikakati ya kuwasaidia wazazi wamudu kusomesha watoto, ila mikakati ya tozo lao

chanzo tanzania daima

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni