Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Alhamisi, 6 Februari 2014

makala kusoma kuhesabu tatizo kubwa kwa wanafunzi nchini

Tangu mwaka 2010, taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza kupitia mradi wake wa Uwezo, imekuwa ikifanya tafiti katika nchi za Afrika Mashariki zinazolenga kubaini uwezo wa watoto wa shule za msingi katika stadi za kusoma na kuhesabu.
Majaribio haya, yamekuwa yakihusisha masomo ya Hesabu na lugha za Kiswahili na Kiingereza kwa ngazi ya darasa la pili. Sampuli hujumuisha wanafunzi wa darasa la tatu na darasa la saba.
Sampuli ya washiriki
Takwimu zinaonyesha kuwa, mwaka 2010 watoto walioshirikishwa kwenye utafii huo walikuwa 37,683 mwaka 2011 wanafunzi 114,761 na mwaka 2012 wanafunzi walioshiriki ni 104,568.
Kwa upande wa kaya, mwaka 2010 zilishiriki kaya 18,952 mwaka 2011 zilikuwa kaya 59,992 na mwaka 2012 kaya. 55,191. Kwa wilaya, mwaka 2010 zilishiriki Wilaya 38, mwaka 2011 zilikuwa wilaya 119 na mwaka 2012 wilaya 126.
Shule zilizoshiriki kwenye utafiti uliofanyika mwaka 2010 zilikuwa ni 1,010 mwaka 2011 zilikuwa 3,709 na mwaka jana zikawa 3,624.
Mratibu wa Uwezo upande wa Tanzania, Zaida Mgalla anasema aghlabu majaribio hayo hutayarishwa kwa pamoja na wataalamu wa masomo kutoka vyuo vikuu, Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na walimu wa masomo husika wa darasa la pili.
Matokeo 2010
Utafiti huu ulipofanywa mwaka 2010 ulionyesha kuwa, japo Kiswahili ni lugha inayozungumzwa kwa upana zaidi nchini, idadi kubwa ya watoto hawawezi kusoma kupitia lugha hiyo.
“Kwenye sampuli zetu, chini ya nusu (42.2 asilimia) ya watoto waliofanyiwa uchunguzi waliweza kusoma kwa hatua ya hadithi. Wakati watoto wote katika darasa la tatu wanapaswa kuweza kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, watoto chini ya mmoja kati ya watatu (32.7 asilimia) ndio wanaweza.
‘’Hata hivyo, hadi wanamaliza shule ya msingi, mtoto mmoja kati ya 5 hawezi kusoma hadithi ya ngazi ya darasa la pili, licha ya kumaliza miaka saba ya elimu ya msingi,”inasema sehemu ya utafiti huo.
Kwa upande wa Kiingereza, ripoti hiyo ya mwaka 2010 inaonyesha kuwa chini ya mwanafunzi mmoja kati ya 10 (7.7 asilimia) ndio anayeweza kusoma hadhithi ya Kiingereza ya ngazi ya darasa la pili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni