Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumatano, 9 Oktoba 2013

Wanafunzi 2,446 hawapati chakula cha WFP






IMEELEZWA kuwa wanafunzi 2,446 waliopo katika shule za msingi za wilayani Bahi, mkoani Dodoma, hawapati chakula kinachotolewa kwa msaada na Shirika la Chakula Duniani (WFP) kutokana na shule hizo kukosa majengo ya kuhifadhi chakula.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Elimu wa Shule za Msingi Bahi, Mary Mathew.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mary alisema ukosefu wa majengo unatokana na wazazi kutokuwa tayari kujitolea kujenga.

Alisema msimamo wa WFP uko wazi kwamba hawako tayari kutoa chakula kwenye shule zisizo na majengo ya kuhifadhiwa chakula.

Alieleza kuwa katika Wilaya ya Bahi, kuna shule za msingi 72 na kati ya hizo shule saba hazipati chakula cha mchana kutokana na wazazi kutoitikia mwito wa kujitolea.

Ofisa Elimu huyo alisema hali ya kukosekana kwa huduma ya chakula kwenye shule hizo imesababisha utoro kwa wanafunzi.

Shule ambazo hazipati chakula cha mchana ni pamoja na Nholi, Bakolo, Chikopelo Nhinyila, Tinai, Mgondo na Bahi Misheni.
 
Chanzo. Marafiki wa elimu dodoma

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni