Kurasa

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania

Jumanne, 29 Julai 2014

Wanafunzi 140 wakwepa masomo tunduma na kujihusisha na biashsra ndogondogo.

Zaidi ya wanafunzi 140 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma wilayani momba mkoani Mbeya bado hawajaripoti shuleni kuanza masomo na badala yake wanadaiwa kujihusisha na biashara ndogondogo kama vile kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani mwa Tanzania na Zambia mjini Tunduma.
Akizungumza kwenye baraza la halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma, mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya momba ambaye pia ni katibu tawala wa wilaya hiyo, Mathias Mizengo amesema kuwa halmashauri ya mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma inakabiliwa na changamoto ya baadhi ya vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu kutoripoti shuleni na hivyo akawataka viongozi wa mamlaka hiyo kuhakikisha vinaja hao wanatafutwa kila mahali walipo na kuwapeleka shuleni.
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Juma Kitabuje amesema kuwa hadi kufikia mwezi juni mwaka huu wanafunzi 144 kati ya wanafunzi 956 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika mji wa Tunduma ndio ambao walikuwa hawajaripoti shuleni kati yao wanafunzi 70 wakiwa ni wavulana na wanafunzi 74 wasichana huku akielezea sababu kubwa ya watoto hao kutohudhuria masomo kuwa ni kutelekezwa na wazazi na kujihusisha na biashara za kuuza karanga na kubeba mizigo mpakani.
 
Kuhusu hatua ambazo zinachukuliwa na mamlaka hiyo kuhakikisha kuwa wanafunzi hao wanaendelea na masomo, mkurugenzi huyo amesema kuwa wazazi wa watoto hao wamefikishwa kwenye baraza la kata na kupewa muda hadi kufikia Agosti 25 mwaka huu kuwasaka watoto wao popote walipo na kuwapeleka shuleni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni