harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jumamosi, 14 Septemba 2013
Jumanne, 10 Septemba 2013
MTIHANI DARASA LA SABA
SERIKALI mkoani Singida imesema haitasita kuwachukulia hatua wazazi
watakaobainika kuwashawishi watoto wao kufanya vibaya katika mtihani wa
kumaliza elimu ya msingi mwaka huu.
Inadaiwa kuwa baadhi ya wazazi hususani wale wa makabila ya wafugaji
wamekuwa wakiwaambia watoto hao kuchora picha za ng’ombe kwenye mtihani
badala ya kuandika majibu ili wasifaulu na kuchaguliwa kuingia
Sekondari kwa ajili ya kuchunga mifugo na wasichana kuolewa.
Katika kipindi ambacho wanafunzi wa madarasa mengine wako majumbani kwa
ajili ya likizo fupi, maandalizi yote muhimu kwa wale wanaofanya
mtihani wa kumaliza elimu ya msingi yamekwisha kamilika.
Hata
hivyo licha ya kuwaandaa vyema wanafunzi wao, baadhi ya walimu
wanaonekana kuwa na hofu ya kufaulisha kutokana na kuwepo tuhuma za
wazazi kutotaka watoto wao waingie Sekondari.
Katika moja ya
mikutano ya hadhara kuhimiza shughuli za maendeleo, Mkuu wa Wilaya ya
Mkalama anakiri kuwa tatizo hilo limekuwa sugu na kuathiri kiwango cha
elimu mkoani Singida.
Pamoja na kukemea Mkuu huyo wa wilaya ya anatoa msimamo wa Serikali juu ya wazazi wa aina hiyo.
Singida ni moja ya mikoa ambayo imefanya vibaya katika matokeo ya
darasa la saba kwa miaka mitatu mfululizo baada ya kufaulisha chini ya
asilimia 50, pamoja na mambo mengine moja ya sababu ikitajwa kuwa
baadhi ya wazazi kutopenda wala kujua umuhimu wa elimu kwa watoto wao.
SERIKALI mkoani Singida imesema haitasita kuwachukulia hatua wazazi watakaobainika kuwashawishi watoto wao kufanya vibaya katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu.
Inadaiwa kuwa baadhi ya wazazi hususani wale wa makabila ya wafugaji wamekuwa wakiwaambia watoto hao kuchora picha za ng’ombe kwenye mtihani badala ya kuandika majibu ili wasifaulu na kuchaguliwa kuingia Sekondari kwa ajili ya kuchunga mifugo na wasichana kuolewa.
Katika kipindi ambacho wanafunzi wa madarasa mengine wako majumbani kwa ajili ya likizo fupi, maandalizi yote muhimu kwa wale wanaofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi yamekwisha kamilika.
Hata hivyo licha ya kuwaandaa vyema wanafunzi wao, baadhi ya walimu wanaonekana kuwa na hofu ya kufaulisha kutokana na kuwepo tuhuma za wazazi kutotaka watoto wao waingie Sekondari.
Katika moja ya mikutano ya hadhara kuhimiza shughuli za maendeleo, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama anakiri kuwa tatizo hilo limekuwa sugu na kuathiri kiwango cha elimu mkoani Singida.
Pamoja na kukemea Mkuu huyo wa wilaya ya anatoa msimamo wa Serikali juu ya wazazi wa aina hiyo.
Singida ni moja ya mikoa ambayo imefanya vibaya katika matokeo ya darasa la saba kwa miaka mitatu mfululizo baada ya kufaulisha chini ya asilimia 50, pamoja na mambo mengine moja ya sababu ikitajwa kuwa baadhi ya wazazi kutopenda wala kujua umuhimu wa elimu kwa watoto wao.
Alhamisi, 5 Septemba 2013
WATANZANIA WATOA MAONI YAO TOVUTI YA WIZARA YA ELIMU
Ukifungua tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, pembeni
kushoto kuna sehemu ya kupiga kura ya maoni kuhusu hali ya elimu nchini.
Kwa maoni yaliyopo mpaka sasa, asilimia 42 ya waliotoa maoni yao-wana
mtazamo kuwa hali ni mbaya; wakifuatiwa na asilimia 35 wenye mtazamo
kwamba 'kuna kitu hakiko sawa'. Maoni hayo yasiyo ya
kuridhisha-yanayofikia asilimia 77 yametumwa na wananchi na wadau
mbalimbali wa elimu kwenye tovuti ya wizara ya elimu. Je, wizara
inayatumiaje maoni haya ya wadau? Big Result ndiyo jawabu?
Ukifungua tovuti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, pembeni kushoto kuna sehemu ya kupiga kura ya maoni kuhusu hali ya elimu nchini. Kwa maoni yaliyopo mpaka sasa, asilimia 42 ya waliotoa maoni yao-wana mtazamo kuwa hali ni mbaya; wakifuatiwa na asilimia 35 wenye mtazamo kwamba 'kuna kitu hakiko sawa'. Maoni hayo yasiyo ya kuridhisha-yanayofikia asilimia 77 yametumwa na wananchi na wadau mbalimbali wa elimu kwenye tovuti ya wizara ya elimu. Je, wizara inayatumiaje maoni haya ya wadau? Big Result ndiyo jawabu?
Jumanne, 3 Septemba 2013
KUWAFUKUZA WANAFUNZI WA KIKE WANAOPATA MIMBA NI KUKATISHA NDOTO ZAO
Hukumu ya hivi karibuni ya
mahakama ya kikatiba imethibitisha kwamba shule haziwezi kuwafukuza
wanafunzi kwa kupata uja uzito.Lakini Afrika Kusini bado inang'ang'ana
kukabliana na suala hilo linalowaathiri wasichana 180,000 kila mwaka.

Daktari Jay-Anne Devjee ambaye ni mkuu wa afya ya akina mama katika hospitali ya King Dinuzulu anasema kwa mara nyingi hulazimika kuwazalisha wasichana kwa njia ya upasuaji, jambo linaloongeza hatari ya kuvuja damu na kuhatarisha maisha ya wazazi hao.
Phumla Tshabalala, mwenye umri wa miaka 16, anamshikilia mwanawe mchanga aliye na umri wa siku moja.Hii ni mara yake ya kwanza kujifungua na anasema ana wasiwasi kuhusu uwezekano wa kumlea mwanawe peke yake.
Anaeleza hajamuona mpenzi wake kwa muda mrefu na licha ya kumuarifu kwamba amejifungua, hakuna mtu kutoka familia ya mpenzi wake aliyekuja kumjulia hali.
Anatoka katika familia maskini, Babake ndiye anayeilisha familia. Yeye ni binti wa mwisho kati ya mabinti watatu na wa kwanza aliyejifungua mtoto, jambo ambalo familia yake bado haijalipokea vyema.
Inakisiwa kuwa kila mwaka wasichana zaidi ya laki moja na themanini nchini Afrika Kusini hushika ujauzito. 180 kati ya wengine 1000, hupata kuwa wajawazito. 36% ya wasichana wenye mimba hufariki kila mwaka kulingana na takwimu za nchi hiyo wakati wanapojifungua.
Mifuko yao ya uzazi huwa bado haijakuwa vyema kiasi cha kubeba mimba na wengi huwa na wakati mgumu sana wanapojifungua , kulingana na daktari Jay-Anne Devjee.
Phumla anapanga kurudi shuleni kwa wakati muafaka ili aweze kufanya mtihani wa mwisho wa mwaka , lakini ana wasiwasi kuhusu vipi atakavyoweza kutimiza majukumu yote mawili ya kuwa mwanafunzi na mzazi pia.
Anasema laitani angesubiri hadi angekuwa mkubwa.

Lakini anajiona kuwa mwenye bahati kwa kuwa yeye na mwanawe ni wazima na wenye afya.
Madakatari wanasema kuna hatari ya kuzaa ukiwa una umri mdogo. Kwa mujibu wa baraza la utafiti wa sayansi ya binaadamu, viwango vya akina mama wanaofariki ni kubwa kwa wasichana kwa asilimia 36 ya vifo katika uzazi kila mwaka licha ya kwamba ni asilimia 8 pekee ya vifo hivyo ndivyo vinavyoripotiwa.
Utafiti unaashiria kwamba wasichana wengi hulazimika kuacha masomo ili kuwalea watoto wao na wengi wao hukosa kurudi kusoma baadaye.
Maafisa wa elimu wanasema katika shule ya upili wa Intshisekelo nje ya mji wa Durban, zaidi ya wasichana 20 walipachikwa mimba katika nusu ya kwanza ya mwaka.
Maafisa nchini humo wana wasiwasi kwamba huenda kushiriki kwa vijana katika ngono bila ya kinga kukaathiri vita dhidi ya HIV/Ukimwi. Mwalimu mmoja anasema mimba ni miongoni mwa sababu kuu pamoja na umaskini zinazochangia nusu tu ya wanafunzi wa kike kumaliza shule.
Kwa mujibu wa sheria, shule hazipaswi kufichua ni wanafunzi gani waja wazito na inasema baadhi ya wasichana huwa na kibarua kigumu cha kificha matumbo yao yanayozidi kukuwa ikwemo kuvaa nguo kubwa na pia kubeba mabegi yao ya shule mbele.
Sheria hiyo ya mwaka 1996 inasema wanafunzi hawapswi kufukuzwa kwa kuwa ni waja wazito lakini shule zinasema wanalazimika kuwafukuza kwa sababu hazijapewa mafunzo ya namna ya kuwasaidia wasichana hao waja wazito.
Jumatano, 28 Agosti 2013
watoto wadogo nchini tanzania wanafanya kazi migodini
Shirika la kutetea haki za kibinadam la Human
Rights Watch, limefichua ushahidi zaidi kuhusu unyanyazaji wa watoto
nchini Tanzania, baadhi yao wenye umri wa miaka minane ambao wanafanya
kazi kwa zamu, katika migodi ya madini iliyoko chini ya ardhi, kwa saa
ishirini na nne.
Shirika hilo limesema watoto hao wanakabiliwa na tishio la kuvuta hewa ya sumu inayotokana na uchimbaji wa madini ya dhahabu na wakati mwingine kuuawa wakati migodi hiyo, inapoporomoka nyingi zikiwa hazina leseni.
Tanzania ina sheria kali inayozuia watoto kufanya kazi katika machimbo ya madini lakini shirika hilo limesema, serikali ya rais Jakaya Kikwete ni sharti iimarishe juhudi zake za kuhakikisha sheria hizo zimetekelezwa.
Shirika hilo limesema watoto hao wanakabiliwa na tishio la kuvuta hewa ya sumu inayotokana na uchimbaji wa madini ya dhahabu na wakati mwingine kuuawa wakati migodi hiyo, inapoporomoka nyingi zikiwa hazina leseni.
Tanzania ina sheria kali inayozuia watoto kufanya kazi katika machimbo ya madini lakini shirika hilo limesema, serikali ya rais Jakaya Kikwete ni sharti iimarishe juhudi zake za kuhakikisha sheria hizo zimetekelezwa.
Jumamosi, 24 Agosti 2013
KUTOKA KWA MARAFIKI WA ELIMU DODOMA
Hiki ni kibao kinacho wakumbusha wanafunzi wa shule ya sekondari Changaa kutumia lugha ya Kiswahili badala ya Kirangi wawapo shuleni hapo. Ajabu ni kuwa Ofisa Elimu Mkoa wa Dodoma eti kamshusha cheo Mkuu wa shule hiyo. Kwa maoni yangu nadhani kushushwa cheo kwa Mkuu huyo wa shule kumekuwa faraja kwake kwani wanafunzi wake hawaongei kiingereza wala Kiswahili badala yake wanatumia KIRANGI.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)




