Baada ya matokeo ya kidato
cha IV mwaka 2013 kutangazwa mwishoni mwa wiki iliyopita , Kumeibuka
maswali yanayohitaji majibu ya kina kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi . Wananchi wangependa kufahamu utaratibu uliotumika kupanga
madaraja kwani kumeibuka mkanganyiko mkubwa usio na majibu mfano kuna
wanafunzi wenye alama 42 wamepewa Division Zero
huku wenzao wenye alama 46 wakipewa Division Four. Pia vyombo vya
habari vimenukuu Shule ya Mtakatifu Francis kuwa kinara katika mitihani
huo ikiwa na Division 1 = 81; Division 2 = 8 , Division 3 =1 , Divison
4= HAKUNA na Division 0= HAKUNA ingawa Shule ya Wavulana ya Marian ina
Division 1= 100, Division 2= 10, Division 3= HAKUNA, Division 4= HAKUNA
na Division 0= HAKUNA . Pengine kuna mambo mengine ambayo yanaleta
mkanganyiko baada ya kupokea matokeo hayo, tutafakari na kuhoji ili
kupata ufafanuzi.
chanzo .haki elimu
harakati za marafiki wa elimu musoma wasiliana nasi kwa namba +255755 650 075 au +255786 650 075 ni jukumu letu kuboresha elimu
HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU NI NINI?
Ni harakati za watu wanaojali na wenye nia ya kuleta mabadiliko katika kuboresha elimu na demokrasia nchini. Harakati hizi zinawaleta pamoja wananchi wanaopenda maendeleo ya elimu na zinawapa fursa ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika masuala yanayohusu elimu .Sera na mipango mbalimbali ikiwemo mpango wa maendeleo ya elimu ya msingi (MMEM) na mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari (MMES) inasisitiza ushiriki wa wananchi katika utekelezaji wake.Hivyo wananchi wote wanawajibu wa kuchangia uboreshaji wa elimu na demokrasia nchini. kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu ni bure na hakuna malipo yoyote wasiliana nasi kwa namba 0755 65 00 75 au 0786 65 00 75 au e-mail jmrchrd@yahoo.com tukuunganishe na marafiki wa elimu popote ulipo Tanzania
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni